Sunday, February 07, 2010

Mzimu wa vitambulisho vya taifa



SAKATA la lililoibua mjadala mkubwa mwaka jana la mradi wa vitambulisho vya taifa na kumlazimu Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati na kuagiza lishughulikiwe kwa haraka huenda likaisha ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Mradi huo wa vitambulisho vya taifa ulioanza maandalizi mwaka 1995 na kupitishwa na kikao cha Bazara la Mawaziri kilichoketi Februari, 2007, hivi karibuni umekuwa unaandikwa zaidi kwenye vyombo vya habari hasa ikiwamo kuachwa kwa Kampuni ya Sagem ya Uswisi katika hatua ya pili ya kuwachuja wazabuni hao.

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo hii, Mkurugenzi Mtendaji wa NIDA, Dickson Maimu (pichani) alisema miradi 14 ndiyo itakayogharimu kiasi cha Sh 200bilioni.

No comments: