WATU 24 akiwamo dereva wa basi wamekufa papo hapo na wengine zaidi 30 kujeruhiwa baada ya mabasi mawili kugongana uso kwa uso katika ajali ilyotokea Kijiji cha Kitumbi Wilayani hapa katika barabara kuu ya Segera - Chalinze.
Kwa mujibu wa habari za awali zilizopatikana na kuthibitishwa na maafisa wa polisi waliokuwepo katika eneo la ajali ni kuwa ajali hiyo ilitokea jana saa 8.50 mchana.
Walioshuhudia ajali hiyo muda mfupi uliopita walisema kuwa ajali hiyo ilihusisha basi la Kampuni ya Chatco iliyokuwa ikitokea Arusha kuelekea Jijini Dar es saalam lililovaana uso kwa uso na basi la Kampuni ya Mzuri Transport ambalo lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Lushoto Mkoa wa Tanga na kwamba walishuhudia maiti nyingi zikiwa zimebebwa ndani ya lori.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TANZANIA YAUNGA MKONO MABADILIKO YA MFUMO WA AFYA DUNIANI
Na Hassan Kimweri, WAF - Addis Ababa Tanzania imeunga mkono juhudi za kuimarisha Shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia maboresho ya Muundo w...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...
No comments:
Post a Comment