Sunday, February 14, 2010

JK atangaza Malaria janga la taifa



RAIS Jakaya Kikwete ameutangaza ugonjwa wa malaria kuwa ni Janga la Taifa na kuwaambia Watanzania kuwa Serikali yake imeanza safari ya kuutokomeza ugonjwa huo nchini. Malaria ndiyo ugonjwa unaoua Watanzania wengi zaidi kuliko mwingine wowote.

Rais Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa marais wanaopambana na malaria barani Afrika alisema kwamba, ugonjwa wa malaria ni vita ambavyo ni lazima Watanzania wavishinde kwa vile nia ipo, sababu ipo na uwezo upo.

Aliongeza kusema kuwa, lengo la serikali ni kuhakikisha kuwa malaria inakuwa ugonjwa wa historia kwa Tanzania kwa kuwa hata nchi nyingine zimefanikiwa kuutokomeza.

Alisema kuwa kila siku ya Mungu, kiasi cha watu kufikia 291 hufariki kwa ugonjwa wa malaria, wengi wao wakiwa watoto wadogo, vifo ambavyo alivielezea kuwa vinaweza kuzuilika na kutibika.

“Kila siku ya Mungu, hapa nchini, wanakufa watu hadi 291 kwa ugonjwa wa malaria. Kwa maneno mengine, kila saa inayopita, wanakufa watu zaidi ya 10 kwa ugonjwa wa malaria.” Rais Kikwete aliliambia taifa usiku wa kuamkia jana.

“Hawa ni watu wengi mno. Hivyo, malaria ni Janga la Taifa letu. Lakini cha kusikitisha zaidi ni kwamba malaria ni ugonjwa unaoweza kuzuilika na kutibika. Ndiyo maana tumeamua kuwa wakati tunaendelea kushughulikia kutibu wagonjwa wa malaria, tuelekeze nguvu zetu katika kuzuia kwa kuanza juhudi za kutokomeza malaria nchini.”

Rais Kikwete alikuwa akizungumza moja kwa moja na taifa wakati anazindua Kampeni dhidi ya Malaria katika burudani maalumu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club mjini Dar es Salaam juzi usiku.

Kampeni hiyo imeanzishwa kwa ushirikiano baina ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii nchini na taasisi za Malaria No More, Population Services International (PSI) na Chuo Kikuu cha John Hopkins, vyote vya Marekani.

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Wabunge wapya wateule wa Rais


Mbunge wa Kuteuliwa, Ismail Jussa Ladhu, akiapa Bungeni Mjini Dodoma juzi ijumaa

Mbunge wa Kuteuliwa, Janet Zebedayo Mbene akiapa Bungeni Mjini Dodoma juzi ijumaa. Picha za Edwin Mjwahuzi.

4 comments:

Anonymous said...

KWANI ALIKUWA HAJUI??????

Anonymous said...

ANGETANGAZA UFISADI NI JANGA LA TAIFA.TUNGEELEWA

Elliott Broidy said...

Beautiful!

Anonymous said...

So the jоіnts may be tantric massagе techniques a
tωosome will be able to achieve simply that. Ιn fact, the next meter Ӏ make іs very brawny and a rendering waѕ intentional for ωomаnhоod.
She's got everything that them in the bowels of the Dry land and in the skies.

My web-site - homepage