Wednesday, May 21, 2008

Balali kafariki dunia




MAMBO ni ya ajabu ajabu kuhusiana na taarifa za Dk Daud Balali, wengine wanasema Mzee Daudi Balali (pichani) amefariki, wengine wanasema amejificha Boston au Washington D.C. huko Marekani!

Kuna habari iliyotoka jana kwenye African Baraza kuwa Mzee Balali anasakwa na wapepelezi kuhusiana na wizi wa dola $133 milioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

Wakati huo huo imethibitishwa hapa Bongo kwa Balali, amefariki dunia.Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Patrick Mombo, alithibitisha kifo hicho baada ya kupata taarifa rasmi kutoka Balozi wa Tanzania Ombeni Sefue.

Balozi Mombo aliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam kwamba, Balozi Sefue alipata taarifa hizo juzi saa 4:00 usiku kwa saa za Marekani.kwa taarifa zaidi soma mwananchi kesho.

No comments: