KATIKA hatua ambayo inaonyesha azma ya kuziba pengo la majaji nchini, Rais Jakaya Kikwete, ameteua majaji 11 wapya ambao saba ni wanawake.
Uteuzi huo wa Rais licha ya kujaribu kuziba pengo la majaji, lakini pia umezidi kuongeza uwiano wa wanawake na wanaume katika nafasi za juu za maamuzi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Ikulu, ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, uteuzi huo umeanza Jumamosi iliyopita, Mei 24, 2008.
Rais amefanya uteuzi huo pia ikiwa ni takriban mwaka mmoja tangu ateue majaji wengine 20, ambao alifanya baada ya bunge la bajeti la mwaka jana.
Luhanjo katika taarifa hiyo ya Ikulu, aliwataja wanawake walioteuliwa kuwa majaji ni Sophia Wambura, Crecencia William Makuru, Zainabu Goronya Muruke na Upendo Hillary Msuya.
Wengine ni Atuganile Florida Ngwala, Rose Aggrey Teemba na Rehema Kiwanga Mkuye.
Majaji wengine wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni Kassim M. Nyangarika, Gabriel Kamugisa Rwakibarila, Ibrahim Sayida Mipawa na Lawrence Kisenge Nziajose Kaduri.
Katibu Mkuu Kiongozi ametangaza pia kwamba, Rais Kikwete amemteua Ferdinand Leons Katipwa Wambali, kuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani.
Wambali anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Wambura ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania.
Kabla ya uteuzi wake, Wambali alikuwa Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment