Thursday, May 22, 2008

Mke wa Ballali asema anamwachia Mungu

WAKATI bado kukiwa na kiwingu kizito katika chanzo cha kifo cha Gavana wa zamani wa Benki Kuu (BoT) Daud Balali, mkewe Anna Muganda, ameunguruma kwamba kilichotokea anamwachia Mungu.

Kauli hiyo ya Muganda ni ya kwanza kuitoa kwa kuzungumza na chombo cha habari cha Tanzania, tangu kutokea kwa msiba wa mumewe.

Muganda katika mazungumzo hayo na mwandishi wa habari hii kutokea Marekani, ambayo yalifanyika jana 1:30 usiku kwa saa za Tanzania ambayo ni asubuhi Marekani, alisema kilichotokea ni mipango ya Mungu.

"Mimi namwachia Mungu, Mungu atajua mwenyewe, tumeshapoa nashukuru sana kwa pole," alisema Muganda, huku akikataa kuzungumza kwa undani kuhusu msiba huo. Kwa taarifa za kina Soma Mwananchi. habari hii inaletwa kwenu kwa hisani ya Ramadhani Semtawa aliyezungumza moja kwa moja na mama Muganda.

No comments:

KASI YA UJENZI WA RELI YA SGR IMEONGEZEKA – PROF. MBARAWA

  Wahudumu wa ndani (Train crew) wa shirika la reli Tanzania (TRC) upande wa Standard Gauge Railway (SGR) wamehudhuria Bungeni Jijini Dodoma...