WAKATI bado kukiwa na kiwingu kizito katika chanzo cha kifo cha Gavana wa zamani wa Benki Kuu (BoT) Daud Balali, mkewe Anna Muganda, ameunguruma kwamba kilichotokea anamwachia Mungu.
Kauli hiyo ya Muganda ni ya kwanza kuitoa kwa kuzungumza na chombo cha habari cha Tanzania, tangu kutokea kwa msiba wa mumewe.
Muganda katika mazungumzo hayo na mwandishi wa habari hii kutokea Marekani, ambayo yalifanyika jana 1:30 usiku kwa saa za Tanzania ambayo ni asubuhi Marekani, alisema kilichotokea ni mipango ya Mungu.
"Mimi namwachia Mungu, Mungu atajua mwenyewe, tumeshapoa nashukuru sana kwa pole," alisema Muganda, huku akikataa kuzungumza kwa undani kuhusu msiba huo. Kwa taarifa za kina Soma Mwananchi. habari hii inaletwa kwenu kwa hisani ya Ramadhani Semtawa aliyezungumza moja kwa moja na mama Muganda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
DKT. MWIGULU AWASILI SONGEA KUSHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA JENISTA MHAGAMA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Desemba 15, 2025 amewasili mjini Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
No comments:
Post a Comment