Wednesday, May 27, 2015

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MANJANO FOUNDATION YAKAMILIKA

 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd. Mama  Shekha Nasser (Katikati)  akizungumza na Vyombo vya Habari jijini Dar es salaam wakati akelezea Mandalizi ya Uzinduzi wa Manjano Foundation Ambao ni Mpango unaolenga kuwawezesha Kutoa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa Wasichana wa Kitanzania. Mpango Uzinduzi huu utafanyika tarehe 31 Mei 2015 kuanzia saa 6 mchana kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Hall. Utatoa fursa kwa kuendeleza mtandao wa kibiashara kwa kina mama na pia mada mbali mbali ya jinsi ya kujikwamua kimaisha itatolewa. Bila ya kusahau mafunzo ya jinsi ya kutumia vipodozi..Mgeni Rasmi anategemewa Kuwa Mke wa Waziri Mkuu Mh Mama Tunu Pinda
 Meneja Mradi wa Manjano Foundation Mama Gugu Ndolvu Akieleza jambo jana wakati wakiongea na wanahabari kuhusu Mradi huo ambao ni Mkombozi kwa wakinamama wasio na Ajira Akiwa samabamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd. Mama  Shekha Nasser  Pamoja na  Aunty Sadaka Gandi
 Aunty Sadaka Gandi akiwa ni dada mkuu wa Atakayewashauri wasichana watakaopata mafunzo ya ujasiriamali kupitia Manjano Foundation. 
Wasichana waliochaguliwa kunufaika na Mpango hup wakiwa Katika Picha ya Pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd. Mama  Shekha Nasser.
…………………………….
Shear Illusions inasherehekea mwongo mmoja wa urembo nchini Tanzania kwa kuzindua
vipodozi vyake ijulikanayo kama LuvTouch Manjano!
Uzinduzi
huu utafanyika tarehe 31 Mei 2015 kwenye Ukumbi wa Diamond
Jubilee VIP Hall. Shamrashamra hizi pia itatoa fursa kwa kuendeleza mtandao wa
kibiashara kwa kina mama na pia mada mbali mbali ya jinsi ya kujikwamua
kimaisha itatolewa. Bila ya kusahau mafunzo ya jinsi ya kutumia vipodozi.
Mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda na mtoa mada mkuu atakuwa
ni Balozi Mwanaidi Majaar.
Shear
Illusions, imeweza kutambulisha urembo na muonekano wa mwanamke wa kitanzania
kwa Zaidi ya miaka kumi. Wamebaisha urembo kuanzia kujipodoa, nywele, vipodozi
na vito hadi blog na jarida inayoelezea masuala ya urembo. Baada ya kuuza
bidhaa mbali mbali ya urembo toka nchi mbali mbali, Shear Illusions inazindua
rasmi bidhaa yake ya LuvTouch Manjano.
LuvTouch
Manjano ni maalum kwa ajili ya kumpendezesha mwanamke wa kitanzania. Kuna aina
kumi ya vipodozi msingi kuanzia Mwanzi na Mpodo hadi kahawa na ardhi. Bidhaa
hizi zimezingatia hali ya hewa ya joto. Vipodozi hivi vinalengo la kuongeza
muonekano wako kwa hali yoyote.
Shear Illusions inazishukuru kampuni zifuatazo waliojitokeza kusaidia hafla hii ya kuwawezesha
wanawake; NSSF, TCRA, Clouds Media, Maxcom, A1 Outdoor, Mr. Price, Cassandra
Lingerie, Amina Design, Maznat Bridal, Advertising Dar, Beauty Point, Hugo
Domingo, I-View Media, FAIDIKA, Benchmark Productions, Fasta Fasta, TENSHI,
Jardin Modeling Agency na mashirika mbali mbali hapa Dar es Salaam.

No comments: