Saturday, May 30, 2015

MWANDISHI WA HABARI MWANDAMIZI ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UDIWANI KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA SONGEA MKOANI RUVUMA


Mwandishi wa Habari mwandamizi Bi. Celesencia Kapinga akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari ambao hawapo pichani wakata alipotangaza nia ya kugombea udiwani kata ya NDILIMALITEMBO Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).
 Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Ruvuma wakiwa pamoja na Mwandishi wa Habari wa gazeti la Majira ambaye ametangaza nia ya kugombea udiwani kata ya Ndilimalitembo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) . Habari na picha na Demasho.com.
……………………………………………………..
WAKATI watu mbalimbali wameanza kujitokeza
kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia vyama vya siasa
mwandishi wa habari  Mwandamizi,  Mkoani
Cresensia Kapinga ametangaza nia ya kugombea udiwani kata ya Ndilima
litembo manispaa ya Songea  Ruvuma.
Mwandishi huyo ametangaza nia yeke ya
kuwania nafasi ya udiwani  mbele ya
waandishi wa habari  kwenye ofisi za
chama cha waandishi wa habari  Mkoa wa
Ruvuma  zilizopo mtaa soko kuu
mkoani  humo.
Amesema kuwa  kabla ya kutangaza nia amejipima na kujiona
anaweza kuongoza kata baada ya kuwa
aligombea nafasi hiyo kupitia viti masalumu mwaka 2010 ambapo kura
hazikutosha.
Akijibu masawali mbalimbali ya Waandishi wa
habari amesema kuwa ameamua kugombea nafasi hiyo baaada ya kuona Changamoto
mbalimbali zinazowakabaili Wananchi Katika Kata hiyo iliyokonje kidogo ya
Manispaa  ya songea hazijafanyiwa kazi. 
‘Ziko Changamoto nyingi zinazowakabili
Wananchi  wa Kata ya Ndilimalitembo bado
hazijafanyiwa kazi,baadhi zikiwa ni Ukosefu wa Zahanati,Shule kukosa Vyoo na
Wananchi kukosa soko la uhakika la kuuza mazao yao ambazo naamini  nikipata
nafasi ya kuwa Mwakilishi wao nitazishughulikia’anasema Bi. Cresensia
Kapinga.
Anasema kuwa kuwa kutokana na  na taaluma yake ya uandishi wa habari ana
uwezo wa kuingia Ofisi yoyote katika Manispaa ya Songea  na kuwasemea Wananchi wa  Kata hiyo hivyo anasema ni fursa  pekee ya Wananchi hao kumpa Fursa ya kuongoza
Kata hiyo.
Kwa upande wa Waandishi wa habari amesema
kuwa  kwa kuwa yeye ni Mwanahabari
atajitahidi kuwasema kwenye Baraza la
Madiwani  akiamini yapo mambo
mengi yanashindwa kushughulikiwa ikiwemo posho zao.
Kwa upande wao Waandishi wa Habari
wamepongeza hatua hiyo  na kutaka
Waandishi wengine wajitokeze kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa kuwa
Waandishi wamekuwa  wakinadi watu wengine
wakati wapo baadhi yao wana uwezo wa kuongoza.
Mmmoja wa Waandishi hao Julius Konala
anasema hatua hiyo ni ya kupongeza sana kwa kuwa imefunguia njia kwa Wanahabari
wengine kugombea zaidi  na kuwata
Wananchi  na Wanaccm kumuunga mkono  katika
azma yake ya kutaka kuwa  Diwani
wa Kata ya Ndilimalitembo.

No comments: