Tuesday, May 26, 2015

PSPF YAUNGANA NA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KATIKA HAFLA YA KUENDELEZA UMOJA WA WAJASIRIAMALI DAR ES SALAAM

  Meneja msaidizi wa uchangiaji wa hiari Matilda Nyallu wa mfuko wa pensheni wa (PSPF) akieleza namna ya mfuko wa Hiari unavyo kuwa na ni jinsi gani utafaidika pindi unapo jiunga na kuwa mmoja wa wadau wa (PSPF)
 Kushoto Muandaaji wa sherehe ya wanawake wajasiliamali Shamimu Mwasha ambaye ni mdau wa (PSPF) akitoa ufafanuzi wa sherehe hiyo na kuwakaribisha wageni walioweza kuhudhuria pembeni ni mshereheshaji wa sherehe hiyo Jokate Mwegelo.
 Baadhi ya wanawake wajasiriamali wakiwa wameketi pamoja huku wakiendelea kupokea ujumbe mbalimbali kutoka kwa wanawake tofauti tofauti waliokuwepo katika sherehe hiyo.
…………………………………………………………………………………………..
Wanawake wajasiriamali Dar es salaam washerehekea pamoja katika hafra fupi iliyo andaliwa na Mjasiriamali Shamimu Mwasha kwa lengo la kuendeleza kuwa na mahusiano mazuri katika shughuli zao za kuijenga nchi kwakutumia  vipaji na ubunifu walionao ili kuhakikisha bidhaa mbalimbali zakitanzania hazikosekani katika soko la hapa nyumbani hata nje ya nchi.

Mfuko wa jamii wa (PSPF) umeweza kuwaunga mkono wajasiriamali hao kwa kuwa miongoni mwa mfuko unaotoa huduma mbalimbali kupitia mafao yao kwakuwa kunamafao mbalimbali katika  mfuko wa pesheni ambayo wao kama wajasiriamali wanaweza kuyamudu na hatimaye kufikia malengo waliyo jiwekea.

Akizungumza wakati wa sherehe hiyo Meneja msaidizi wa uchangiaji wa hiari Matilda Nyallu amesema mfuko wa jamii wa (pspf) ni mfuko unao jali kila mmoja na nimfuko ambao unakupatia wewe mtanzania faida maradufu kutokana na huduma zinazo tolewa kuwa za kiwango cha hali ya juu amesema kupitia mafao mbalimbali likiwemo fao la mikopo ya elimu,fao la ujasiriamali,nyumba na mengine mengi pia aliweza kuwaeleza kuhusu uchangiaji wa hiari ambapo kupitia uchangiaji huo mtu yeyyote anaweza akaumudu kutokana ni rahisi na inakiwango cha kawaida cha kuchangia .

No comments: