Sunday, May 31, 2015

STEPHEN WASSIRA ATANGAZA NIA YA KUWANIA URAIS


Stephen Wassira akitangaza nia ya kuwania Urais kwenye Ukumbi wa wa BOT jijini Mwanza leo.
WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira leo ametangaza nia ya kuwania Urais kwenye Ukumbi wa wa BOT jijini Mwanza.
Wassira anawania nafasi ya kugombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Katika hotuba yake wakati wa kutangaza nia yake, Wassira amesema amepata kuteuliwa kuongoza sehemu mbalimbali nchini maana marais wote wa awamu nne walikuwa na imani naye.
Pia amewashukuru wageni waalikwa waliofika kwenye ukumbi kutoka sehemu mbalimbali kwa kuweza kufika na kumuunga mkono huku wakiwa na imani naye.
Kauli mbiu yake ni katika mbio hizo ni Uchumi Imara kwa Tanzania mpya.

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...