Monday, April 27, 2015

NHBRA WAMEGUNDUA NJIA RAHISI YA KUTENGENEZA VIGAE VYA KUPAULIA NYUMBA

   Meneja  wa Utafiti na Maendeleo wa NHBRA Injinia Elias Kwemana akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari MAELEZO Ajijini Dar es Salaam leo kushoto ni kaimu afisa Habari wa NHBRA Frimin Lyakurwa kulia ni  Afisa masoko  wa NHBRA Zubeda Salum.
  Meneja  wa Utafiti na Maendeleo wa NHBRA Injinia Elias Kwemana akionyesha aina  ya kwanza ya kigae  cha kupaulia nyumba,kushoto ni kaimu afisa Habari wa NHBRA Frimin Lyakurwa kulia ni  Afisa masoko  wa NHBRA Zubeda Salum.
 Meneja  wa Utafiti na Maendeleo wa NHBRA Injinia Elias Kwemana akionyesha aina  ya pili ya kigae  cha kupaulia nyumba,kushoto ni kaimu afisa Habari wa NHBRA Frimin Lyakurwa.

  Baadhi ya wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa kuonyesha aina mbalimbali za vigae vinavyoweza kutengenezwa na kila mwananchi hapa nchini katika ukumbi wa Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)
 
Na Avila Kakingo,Globu ya Jami.
WAKALA Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA) wamegundua njia rahisi ya kuboresha makazi kwa kutumia vigae kwa gharama nafuu ambazo kila mwananchi anaweza kuzimudu. 

Hayo yamesemwa na  Meneja  wa Utafiti na Maendeleo wa NHBRA Injinia Elias Kwemana akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari MAELEZO jijini Dar es Salaam leo.
 Kwemana amesema kuwa utengenezaji wa vigae hivyo ni rahisi na gharama hafuu kwani bidhaa zote za kutengeneza vigae hivyo zinapatikana hapa hapa  nchini.
Hifaa hivyo  vinavyotumika kutengenezea vigae hivyo ni mchanga sementi na  nyuzi za katani bidhaa  hizo zote zinapatikana hapahapa nchini, ikiwa kuna  mashine inayotumika kushindilia mchanga uliochanganywa na sementi nayo ni gharama nafuu ukilinganisha na faida zinazopatikana.
Kwemana amesema kuwa  njia ya kutengeneza vigae hivyo vitasaidia  kutumika kama njia nyingine ya kupaua nyumba zetu ambapo vigae hivyo huu kaa muda mrefu kuliko kutumia Nyasi au Bati.

No comments: