Friday, April 17, 2015

IGP ERNEST MANGU AKIZUNGUMZA NA MASHEIKH

1
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akiongozana na viongozi wa dini ya kiislamu (kulia) Mwakilishi wa Mufti wa Tanzania katika Mafunzo hayo Sheikh Abubakar Zuber na kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwinyibaraka Sheikh Issa Othman wakati akilelekea kufungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo Viongozi wa dini ya Kiislamu ili kuimarisha usalama nchini.Mafunzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Mwinyibaraka na kufanyika jijini Dar es Salaam juzi.
(Picha na Frank Geofray wa Jeshi la Polisi)
2
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akizungumza na viongozi wa dini ya kiislamu waliohudhuria katika mafunzo ya kuwajengea uwezo Viongozi wa dini hiyo.Mafunzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Mwinyibaraka na kufanyika jijini Dar es Salaam juzi.
3
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akizungumza na Katibu wa Jumuiya ya Wanazuoni wa kiislamu Sheikh Khamisi Mataka katika Mafunzo ya kuwajengea uwezo Viongozi wa dini ya Kiislamu ili kuimarisha usalama nchini.Mafunzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya Mwinyibaraka na kufanyika jijini Dar es Salaam juzi.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...