Friday, April 17, 2015

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI(MUWSA) YAKAMATA WEZI WA MAJI

Watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika nyumba moja ambayo inadaiwa mmiliki wake alikuwa akiiba maji baada ya kujiunganishia kinyemera licha ya kukatiwa huduma hiyo kwa muda mrefu.
Wafanyakazi hao wakiongozwa na afisa uhusiano wa mamlaka hiyo ,Frolah Nguma na mkuu wa kanda ya Rau ,Selemani Zabron na fundi Aminiel Swai baada ya kufuatilia katika eneo hilo walibaini wapi wizi wa maji unafanyika.
Hivi ndivyo ilivyooonekana katika mauongio ya mteja wa mamlaka hiyo ambaye mtuhumiwa wa wizi wa maji alifanya usanii wa kujiungia maji bila ya kulipia huku mzigo wa kulipia ankala ya maji ikibaki kwa jirani yake aliyeunganisha bomba kwenye line yake.
Fundi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Aminiel Swai akiondoa bomba liliunganishwa kwa wizi .
Mkuu wa kanda ya Rau wa mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi Selemani Zabron akifukia eneo ambalo hujuma ya kujiunganishia maji ilikuwa imefanyika.
Mmiliki wa nyumba hii ndiye line ya kupeleka maji kwake imekutwa ikiwa imefanyiwa hujuma na kulazimika kulipa bili ya matumizi ya maji kwa nyumba mbili.
Watumishi wa MUWSA wakitazama kama maji yanatoka katika nyumba hiyo mara baada ya kuondoa bomba ambalo lilikuwa likitumika kupeleka maji katika nyumba nyingine kwa njia ya wizi.Hata hivyo katika operersheni hiyo Mtuhumiwa pamoja na mkewe walilazimika kuikimbia nyumba yao na kutelekeza watoto wao wawili wakiume wenye umri wa kati ya miaka miwili na minne.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: