Friday, April 17, 2015

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ,LEONIDAS GAMA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA KILIMANJARO.


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akizungumza wakati alipokutana na wafanyabiashara katika viwanja vya Kili Homes mjini Moshi kuzungumzia kero mbalimbali zinazowakabili pamoja na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazo wakabili.kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga.
Baadhi ya wafanyabiashara wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro katika mkutano huo.
Mjumbe wa kamati maalumu ya kuratibu kero za Biashara mkoa wa Kilimanjaro Patrick Boisafi akisoma kero zilizoratibiwa mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama.
Baadhi ya wafanyabiashara.
Katibu wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania ,tawi la Kilimanjaro,Mmasi Sambuo akisoma kero mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara Kilimanjaro mbele ya mkuu wa mkoa.
Wafanyabiashara wakifuatilia mkutano huo.
Add caption

Mfanyabiashara Ibrahim Shayo akitoa kero mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati wa mkutano wa wafanyabiashara,maofisa wa TRA,manispaa ya Moshi pamoja na mawakala wa mashine za EFD'S ulioongozwa na mkuu wa mkoa Leonidas Gama
Baadhi ya wafanyabiashara wakitoa kero zao.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ,TRA mkoa wa Kilimanjaro Abdul Mapembe akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali pamoja na kero zilizoibuliwa na wafanyabiashara wakati wa mkutano huo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: