Monday, April 20, 2015

Edward Lowassa ashiriki Matembezi ya kupiga vita mauaji ya watu wenye Ualbino


















Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Mh. Edward 
Lowassa (katikati mwenye kapelo), "akitroti" kukimbia sambamba
na mamia ya watu waliojitokeza kwenye matembezi ya kuunga
 mkono kupiga vita dhidi ya mauaji ya watu wenye Ualbino,
yaliyofanyika jana kuanzia Uwanja wa Taifa na kuishia kwenye
Viwanja vya TCC Club, Chang'ombe jijini Dar es salaam. Katika
hotuba yake mwishoni mwa matembezi hayo ya kilomita 5,
 Lowassa alimuomba Rais Jakaya Kikwete, "kumwaga" wino,
ili kubariki hukumu ya kifo dhidi ya waliohusika na mauaji ya Albino.




















Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Mh. Edward
Lowassa (katikati) akishiriki matembezi ya kuunga mkono kupiga
vita dhidi ya mauaji ya watu wenye Ualbino, yaliyofanyika jana
kuanzia Uwanja wa Taifa na kuishia kwenye Viwanja vya TCC
Club, Chang'ombe jijini Dar es salaam.Kushoto ni Mbunge wa
Ilala, Mh. Mussa Zungu.
Michuzi 

No comments:

NHC YATOA ELIMU YA HATI PACHA, YASISITIZA UMOJA WA WAMILIKI SAMIA HOUSING SCHEME KAWE

 Samia Housing Scheme Kawe: nyumba 560, familia tofauti zikiunganishwa na mtindo mmoja wa maisha ya  kisasa—ushirikiano, ustaarabu na “moder...