Monday, December 09, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHITIMISHA MBIO ZA UHURU (UHURU MARATHON) KWENYE VIWANJA VYA LEADERS CLUB, KINONDONI DAR

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa Tamasha la kuhitimisha Mbio za Uhuru (Uhuru Marathon) zilizomalizikia kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara, akizungumza kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais Dkt. Bilal kuhitimisha Tamasha la mbio hizo za Uhuru Marathon, kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya wananchi waliohudhuria tamasha hilo la hitimisho la mbio za Uhuru Marathon.
 Sehemu ya wananchi waliohudhuria tamasha hilo la hitimisho la mbio za Uhuru Marathon.
 Sehemu ya wananchi waliohudhuria tamasha hilo la hitimisho la mbio za Uhuru Marathon.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimvisha Medali ya Shaba mshindi wa tatu Kilometa 21 wa Mbio za Uhuru (Uhuru Marathon 2013) Kasirini Renchi, ambaye ni askari Magereza, wakati wa Tamasha la kuhitimisha Mbio za Uhuru Marathon 2013, zilizomalizikia Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimvisha Medali ya Dhahabu mshindi wa kwanza Kilometa 21 wa Mbio za Uhuru (Uhuru Marathon 2013) Jaqueline Juma, ambaye ni askari wa JWTZ Arusha, wakati wa Tamasha la kuhitimisha Mbio za Uhuru Marathon 2013, zilizomalizikia Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
  Washindi wa Mbio za Uhuru Marathon 2013, wa Kilometa 21 mshindi wa kwanza Jaqueline Juma, Askari wa JWTZ Arusha (katika) wa pili Angela Temo, kutoka Kenya (kushoto) na wa tatu Kasirini Renchi, Askari Magereza, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa zawadi zao na Medali kwa kutangazwa washindi wa mbio hizo zilizohitimishwa leo na Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimvisha Medali ya Dhahabu mshindi wa kwanza wa Kilometa 42 kwa upande wa wanaume mbio za Uhuru (Uhuru Marathon 2013) Jamini Ikai, kutoka nchini Kenya, wakati wa Tamasha la kuhitimisha Mbio za Uhuru Marathon 2013, zilizomalizikia Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki wa Mbio hizo wakimalizia katika pointi ya mwisho katika Viwanja vya Leaders. 
 Baadhi ya washiriki wa Mbio hizo wakimalizia katika pointi ya mwisho katika Viwannja vya Leaders. 
 Washindi wa Mbio za Uhuru Marathon 2013, wa Kilometa 42 mshindi wa kwanza, Jamini Ikai, kutoka Kenya (katika) wa pili Steven Sylvester, kutoka Tanzania (kushoto) na wa tatu Alex Sanka wa Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa zawadi zao na Medali kwa kutangazwa washindi wa mbio hizo zilizohitimishwa leo na Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Meza Kuu ikifurahia na kuwapongeza washiriki……..

No comments: