Friday, December 06, 2013

Makamba aongoza uzinduzi wa Azam TV


 Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba (MB) akizungumza kwenye uzinduzi wa Azam TV uliofanyika Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel mwishoni mwa Juma ambapo amesema Azam TV imekujali kuleta mapinduzi katika ulimwengu wa Digitali na kutoa fursa ya ajira kwa Vijana wa Tanzania wenye vipaji sanjari na kuitangaza nchi yetu katika bara la Afrika hasa kwenye upande wa Soka na Filamu.


Azam TV itaanza kurusha matangazo yake Desemba 6 mwaka huu, Watanzania kaeni mkao wa kula kupata King’amuzi kwa bei rahisi ambacho kitakuwa na chaneli zisizopungua 50.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Tv, Rhys Torrington akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Azam Television jijini Dar es Salaam mwishoni mwa Juma.
 Naibu waziri Januari Makamba akifuatilia maelezo ya awali ya Azam TV

 Wadau mbalimbali na wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi huo wa Azam TV.
 Mkurugenzi wa vipindi wa Azam Tv Efe Atiyio akifafanua juu ya program mbalimbali za Azam Tv


Wadau katika uzinduzi
 Wasiwasi Mwabulambo akiwa na wafanyakazi wenzake wa Azam TV
 Januari Makamba, akitoa neno
 Wageni waaalikwa
Lucy Ngongoseke Kihwele (kulia)akiwa katika pozi na dada yake
 Huu ndio ungo wa Azam TV
 Uzinduzi ndio huooo
Staff wa Azam Media wakiwa wameshika vifaa vya Azam TV
 Mkurugenzi Mkuu wa makampuni ya SSB Ltd. Said Muhammad Said (kushoto) akielezea ubora wa Kisumbuzi cha Azam Tv kwa mmoja wa waalikwa.
Wasanii wa Filamu nchini nao walihudhuria uzinduzi huo wa Azam TV, toka kushoto ni Natasha, Monalisa na Hemed wakiwa na mdau mwingine wakiangalia kipeperushi cha Azam TV.

No comments: