Monday, December 09, 2013

IGP MWEMA ATEUA MAKAMANDA WA MWANZA, MBEYA NA SIMIYU

mwema
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
Aidha, Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Jafary Ibrahim amehamishiwa Kanda Maalum ya  Dar es Salaam  kuwa Mkuu wa Upelelezi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Rogathe Mlasani kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.
Wengine ni Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) David Mnyambuga kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam anaenda kuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Tabora, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Martin Otieno kutoka Kanda Maalum ya Dar es salaam  amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi kuwa Mkuu wa kitengo cha Teknohama na Mrakibu wa Polisi (SP) Gidion  Msuya ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Upelelezi  wa mkoa wa Tarime Rorya amehamishiwa  Tunduru kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD).
Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

No comments: