Tuesday, December 17, 2013

KIJIJI CHA QUNU ALIKOZIKWA MZEE NELSON MANDELA JUMAPILI DESEMBA 15, 2013

 Daraja la waendao kwa miguu likipita juu ya barabara mpya ya lami inayojengwa kuelekea kijijini Qunu.
Siku ya mazishi barabara ya kuelekea Qunu ilifungwa na ni magari yaliyokuwa na kibali tu ndiyo yaliyoruhusiwa kupita
Ulinzi ulikuwa mkali kila sehemu kijijini Qunu
Wageni wakiwa katika geti kuu la nyumba ya Mzee Mandela hapo Qunu
Nyumba ya Mzee Mandela
Nyumbani kwa Madiba kijijini Qunu
Hema maalumu zilikofanyika shuguli zote za mazishi. Kaburi lake liko nje ya hema upande wa kushoto
Hali ilivyokuwa saa kumi na moja alfajiri siku ya Jumapili
Nyumbani kwa Madiba kumejaa magari hata kabla ya jua kupanda angani
Sehemu ya kijiji cha Qunu. Mahema mbele ya nyumba ni ya wanahabari wa kimataifa waliopiga kambi hapo
Mandhari ya Qunu
Mandhari ya Qunu
Ni kijiji chenye mandhari nzuri. Wakati wa majira ya baridi barafu huanguka hapa
Qunu
Kila engo Qunu inapendeza
Kijiji cha Qunu
Bango linalotangaza kijiji cha Qunu kuwa cha urithi
Ulinzi ulikuwa si wa kawaida siku ya mazishi
Foleni ilikuwa ya kufa mtu
Wana Afrika Kusini toka kila kona walitembea umbali mrefu kwa miguu kuhudhuria mazishi
Nyimbo na ngoma vilitawala
Mdau aklipoza koo baada ya kutembea kwa muda mrefu
Sehemu ya mji wa Mthatha, kilomita kama 32 kutoka Qunu
Magari yalizuiwa kwa muda wakati mwili wa Mzee Madiba uliopowasili uwanja wa Mthatha na kupelekwa Qunu
Sehemu ya foleni ya magari ikikaribia mji wa Mthatha na hapa wakisubiri msafara wa mwili wa Mzee Mandela upite
--- 
Qunu ni kijiji kidogo katika jimbo la Eastern Cape la Afrika Kusini, kilomita 32 Kusini-Magharibi ya mji wa Mthatha, katika barabara ya Butterworth na Mthata. 
Kijiji cha Mvezo, pembezoni mwa mto Mbashe, ni jirani ya mahali ambapo Mzee Nelson Mandela alizaliwa. Hapo Qunu ndipo alipokulia na aliweka nadhiri ya kurejea. 
Kijiji cha Qunu ndipo baba yake Mandela alipohamia baada ya kuvuliwa Uchifu wa Mvezo. Katika kitabu chake cha ‘Long Walk to Freedom’ Mzee Mandela amekitaja kijiji hicho kuwa ndipo alipoishi maisha ya furaha wakati wa utotoni. 
Jumapili ya Desemba 15, 2013 Mzee Mandela alizikwa kijijini Qunu katika mazishi ya Kitaifa yaliyoshuhudiwa dunia nzima. Alizikwa kwa heshima zote za kiongozi wa Taifa katika sehemu aliyochagua mwenyewe kuwa nyumba yake ya milele.

No comments: