Tuesday, December 31, 2013

JAMAA AKWEA JUU YA MNARA WA SIMU UBUNGO AKATAA KUSHUKA HADI AONANE NA RAIS HATIMAYE ASHUSHWA

 
Jamaa mmoja ambaye jina lake halijaweza kupatikana leo majira ya saa 5 na nusu asubuhi alipanda juu ya mnara wa kampuni ya simu Vodacom mkabala na ofisi ya Tbs,alipokuwa juu ya mnara alikua na picha pamoja na document mbalimbali ambazo alisema hashuki mpaka Rais Jakaya Kikwete afike eneo hilo.

Baadhi ya mashuhuda wanasema kuwa jamaa ni mpiga debe maeneo ya ubungo na madai yake alifungwa jela miaka 6 bila hatia hivyo moja ya sababu zilizofanya apande juu na kuhitaji kuonana na rais kwa ajili ya kuzungumza nae.
 



Kikosi cha Zimamoto na uokoaji walifanikiwa kumshusha majira ya mchana huu na kumpeleka moja kwa moja kituo cha polisi.

No comments:

SAMIA APEPERUSHA BENDERA YA USHIRIKIANO EAC, AKUTANA NA KATIBU MKUU IKULU CHAMWINO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ...