Thursday, December 05, 2013

AIRTEL YATANGAZA WASHINDI WA DROO YA WIKI YA PILI WA PROMOSHENI YA MIMI BINGWA

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, (Katikati) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kumtangazi Rashid Jacob Kagomola, mkaazi wa Bukoba mkoani Kagera, kama mshindi wa pili wa tiketi mbili na safari ya kwenda kuangalia mechi ya klabu ya Manchester United moja kwa moja (live) nchini Uingereza kwenye uwanja wa Old Trafford wakati wa droo ya wiki ya pili ya ‘Mimi Ni Bingwa’ iliyochezeshwa jana. Kulia ni Ofisa Huduma Kwa Wateja Airtel Pamela Marinyo na Emmanuel Ndaki, Msimamizi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ya Tanzania.…
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, (Katikati) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kumtangazi Rashid Jacob Kagomola, mkaazi wa Bukoba mkoani Kagera, kama mshindi wa pili wa tiketi mbili na safari ya kwenda kuangalia mechi ya klabu ya Manchester United moja kwa moja (live) nchini Uingereza kwenye uwanja wa Old Trafford wakati wa droo ya wiki ya pili ya ‘Mimi Ni Bingwa’ iliyochezeshwa jana. Kulia ni Ofisa Huduma Kwa Wateja Airtel Pamela Marinyo na Emmanuel Ndaki, Msimamizi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ya Tanzania.
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, (Katikati) akimpigia simu Rashid Jacob Kagomola, mkaazi wa Bukoba mkoani Kagera, aliyeibuka mshindi wa pili wa tiketi mbili na safari ya kwenda kuangalia mechi ya klabu ya Manchester United moja kwa moja (live) nchini Uingereza kwenye uwanja wa Old Trafford wakati wa droo ya wiki ya pili ya ‘Mimi Ni Bingwa’ iliyochezeshwa jana. Kulia ni Ofisa Huduma Kwa Wateja Airtel Pamela Marinyo na Emmanuel Ndaki, Msimamizi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ya Tanzania.
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, (Kusoto) akimpigia simu Rashid Jacob Kagomola, mkaazi wa Bukoba mkoani Kagera, aliyeibuka mshindi wa pili wa tiketi mbili na safari ya kwenda kuangalia mechi ya klabu ya Manchester United moja kwa moja (live) nchini Uingereza kwenye uwanja wa Old Trafford wakati wa droo ya wiki ya pili ya ‘Mimi Ni Bingwa’ iliyochezeshwa jana. Kulia ni Ofisa Huduma Kwa Wateja Airtel Pamela Marinyo.
Airtel yatangaza washindi wa droo ya wiki ya pili wa promosheni ya Mimi Bingwa
Kagomola aibuka mshindi wa tiketi ya pili ya Airtel kwenda Old Trafford
KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel imemtangaza Rashid Kagomola, mkazi wa Bukoba mkoani Kagera kama mshindi wa tiketi mbili na safari iliyolipiwa ya kwenda kuangalia moja kwa moja (live) mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza katika uwanja wa Old Trafford.
Kagomola alishinda safari hiyo wakati wa droo ya kila wiki ya promosheni ya ‘Mimi Ni Bingwa’ inayolenga kuwazawadia wateja waaminifu, iliyoingia katika wiki ya pili.
Anakuwa mshindi wa pili wa tiketi baada ya Dickson Lyatuu kutoka mkoani Arusha, kuibuka mshindi wa kwanza.
Akitangaza mshindi wa tiketi hiyo katika wiki ya pili, washindi wawili wa shilingi milioni 5 na washindi wanne wa shilingi milioni moja kila mmoja, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema washindi wote wa tiketi watapewa nafasi ya kuchagua mtu mmoja watakaesafiri nae kwenda Uingereza, kuangalia mechi ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford.
“Tunafuraha kutangaza kuwa mshindi wetu wa tiketi ya kweneda Old Trafford wa droo yetu ya pili ya promosheni ya ‘Mimi Ni Bingwa’ kuwa ni Rashid Jacob Kagomola atakaeungana na Bw. Dickson Lyatuu aliyeshinda tiketi ya kwanza na wengine 11 watakaojishindia tiketi baadae kwenda kuangalia mechi moja kwa moja (live) katika uwanja wa Old Trafford katika mwezi huu wa kwanza wa droo yetu.
“Kagomola alichaguliwa baada ya namba ya mtu wa kwanza kujitokeza, kushindwa kupokea simu baada ya kumpigia mara tatu. Kwa maana hiyo napenda kumuasa kila aliyejisajili katika droo hii kujiweka tayari kupokea simu kutoka Airtel kwa sababu anaweza kuibuka mshindi,” alisema Mmbando.
Aliwataja Godfrey David Msiu kutoka Arusha na Junior Ashery Pesambili, mkazi wa Arusha mjini kuwa washindi wa shilingi milioni tano kila mmoja wa wiki hii na wateja wengine wanne waliojishindia shilingi milioni moja kila mmoja.
Mmbando alisema kuwa bado zawadi nyingi zaidi kushindaniwa na kuongeza kuwa ili kushiriki katika promosheni hiyo mteja anatakiwa kutuma ujumbe mfupi (SMS) ukiwa na neon “BINGWA’ kwenda namba 15656.
Alisema kuwa Airtel pia imeweka vituo maalum kwa ajili ya wapenzi wa Man U kuangalia mechi za Manchester United bure kupitia luninga kubwa, na kuyataja maeneo hayo kuwa, Mbeya – Shaba Pub, Mwanza – Shooters Pub, Dodoma – Four Ways, Dar es Salaam – Rose Garden, Morogoro – Nyumbani Lounge na mkoani Arusha ni Empire Sports Bar.
Droo hiyo ilishuhudiwa na wawakilishi kutoka katika Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ya Tanzania.

No comments: