Saturday, January 05, 2013

WAZIRI Bernard Membe: Sitagombea tena nafsi hii ya ubunge


WAZIRI wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe 
----
WAZIRI wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ametangaza kuwa hatogomea tena ubunge katika uchaguzi mkuu ujao.

Membe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza kwenye sherehe za Mwaka Mpya nyumbani kwake.

“Unajua nimekuwa mbunge wenu kwa kipindi cha tatu. Hivi leo ninawaaga rasmi kuwa sitagombea tena nafsi hii ya ubunge,” alisema Membe.

Ambapo pia aliwataka wananchi wa mikoa ya kusini, kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo Serikali inashughulikia mchakato wa kuvuna gesi asilia.Alisema kuwa ni muhimu kwa wakazi wa mikoa iliyopatikana gesi kutambua kuwa rasilimali zilinazopatikana nchini ni mali ya Watanzania wote na siyo ya  mikoa iliyogundulika pekee.

Waziri Membe aliwataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, kuacha kutumia vikao vya halmashauri kujadili malumbano yasiyokuwa na msingi akisema kwamba kufanya hivyo ni kipoteza rasilimali za wananchi bila faida.Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea.......
SOURCE: http://haki-hakingowi.blogspot.com

No comments: