Wednesday, January 30, 2013

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA:UWEZEKANO WA MATUKIO YA MVUA KUBWA NCHINI KUTOKANA NA KUWEPO KWA KIMBUNGA ''FELLENG''




Tafadhali pokea taarifa hii kuhusu uwezekano wa matukio ya Mvua kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kila siku) katika baadhi ya maeneo ya mikoa  ya Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara  na maeneo jirani ya mikoa hiyo kati ya tarehe 30 Januari, 2013 hadi 01 Februari, 2013.
Hali hii inatokana na kuwepo kwa kimbunga “FELLENG” kaskazini-mashariki mwa Madagascar ambacho kinavuta upepo wenye unyevunyevu kutoka Congo kupitia maeneo tajwa.

Ahsante

Public Weather Service,
 Tanzania Meteorological Agency.
Ubungo Plaza,
Morogoro Road, P.O.Box 3056,
 Dar es Salaam:
Tel: +255 22 2460706-8;Fax: +255 22 2460735
 :Website: www.meteo.go.tz 

No comments: