Friday, January 11, 2013

Mwanri akagua barabara Manispaa ya Sumbawanga

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akipima kwa tape maalum urefu wa moja ya barabara zilizojengwa na Manispaa ya Sumbawanga katika Mji huo kuhakikisha kama barabara hiyo imejengwa kwa vipimo vilivyoanishwa kwenye mpango wa ujenzi huo (BOQ). Naibu Waziri huyo alitumia fursa hiyo kuziasa halmashauri zote nchini kusimamia vyema fedha za Serikali katika miradi kuhakikisha inafanana na thamani ya fedha zilizotumika, alilazimika kusema hayo baada ya kubaini mapungufu mbalimbali katika mradi huo wa barabara na miradi mingine aliyofanikiwa kuitembelea Mkoani Rukwa.

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akikagua barabara za lami zilizo chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga zilizojengwa hivi karibuni. Katika ukaguzi huo alibaini mapungufu mbalimbali katika ujenzi huo na kuagiza Halmashauri hiyo kuhakikisha mapungufu hayo yanaondolewa. Aliitaka pia halmshauri hiyo kusimamia vyema kazi za Serikali kuepusha minong’ono inayotoka kwa wananchi juu ya utendaji mbovu wa baadhi ya watendaji Serikalini.
Mhe. Agrey Mwanri akiweka jiwe la msingi kiwanda cha unga cha Malangali kinachomilikiwa na muwekezaji wa ndani mapema hivi leo. Kwa sasa Mkoa wa Rukwa una viwanda vitatu vya unga vinavyomiliwa na wawekezaji wa ndani.  
Naibu wa Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Agrey Mwanri akikagua kiwanda cha unga cha Malangali Mjini Sumbawanga leo alipotembelea kiwandani hapo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi.
Mhe. Mwanri akizungumza na wakazi wa Mji wa Sumbawanga katika Stendi kuu ya mabasi ya Mjini hapo ambapo alipokea kero mbalimbali ikiwepo ubovu wa miundombinu ya umeme na barabara katika stendi hiyo. Aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Sumbawanga kufanya Mkutano wa hadhara na wananchi hao kuskiliza kero zao zote pamoja na kuzitaftia ufumbuzi na kumpelekea taarifa ya utekelezaji.
Katika hali isiyotegemewa msafara wa Mhe. Mwanri ulipowasili katika kijiji cha Mlanda katika Manispaa ya Sumbawanga kwa ajili ya Mkutano wa hadhara ulikuta msiba ambapo walishiriki na kutoa ubani ambapo Mhe. Mwanri alitoa laki moja na alfu mbili na aliyekuwa Mbunge wa Sumbawanga Mjini CCM ambaye pia ni Mjumbe wa halmashauri kuu Taifa ya CCM (NEC) kupitia Mkoa wa Rukwa Aeshi Hillal alikabidhi shilingi alfu hamsini. 
(Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa – rukwareview.blogspot.com)

No comments: