Thursday, January 10, 2013

AZAM YAIKUNG'UTA SIMBA NA KUTINGA FAINALI YA KOMBE LA MAPINDUZI


Humphrey Mieno wa Azam aliyeenda hewani kuifungia bao la kwanza timu yake

Wachezaji wa Azam, Ibrahim Mwaipopo kushoto na Uhuru Suleiman kulia wakimdhibiti kiungo wa Simba SC, Ramadhani Singano 'Messi' katikati huku kocha wake Jamhuri Kihwelo 'Julio' kulia kabisa akishuhudia

Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
AZAM FC imeingia Fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku huu, baada ya kuifunga Simba SC kwa penalti 5-4, kufuatia sare ya kufungana mabao 2-2 ndani ya dakika 120 usiku huu kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani hapa.
Hadi mapumziko, Azam FC walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na kiungo Mkenya, Humphrey Mieno dakika ya 10, akiunganisha kwa kichwa kona maridadi iliyochongwa na kiungo mzalendo, Ibrahim Mwaipopo.
Azam ilishambulia zaidi baada ya bao hilo, kabla ya Simba kuzinduka dakika tatu baadaye na kuanza kushambulia pia.
Mchezo huo ulisimama kwa dakika tano kuanzia ya 14 hadi 19 kutokana na umeme kukatika uwanjani hapo, hali iliyolazimisha kuwashwa kwa Jenereta.
Kipindi cha pili Simba walibadilika mno kiuchezaji na kuanza kutawala mchezo jambo ambalo liliwasaidia kupata bao la kusawazisha dakika ya 78, ambalo lilifungwa na Rashid Ismail. PICHA NA HABARI KUTOKA kwa http://bongostaz.blogspot.com/2013/01/simba-na-azam-katika-picha-usiku-huu.html
 

Wachezaji wa Azam wakimpongeza Humphrey Mieno kufunga bao la kwanza


Kuna wakati ilibidi Stewart Hall aombe ushauri kwa mchezaji wake wa akiba, Luckson Kakolaki kushoto ambaye anamuambia cha kufanya, bila shaka ilikuwa ushauri mzuri na ndiyo maana timu ilishinda.


Shujaa wa Azam, Malikqa Ndeule akiwa amebebwa juu juu.

No comments: