Sunday, July 20, 2008

Zimbabwe yaanzisha noti ya bilioni 100



BENKI Kuu ya nchini Zimbabwe imeingiza katika mzunguko noti za dola ya Zimbabwe bilioni 100 . Januari mwaka huu Zimbabwe iliingiza katika mzunguko dola ya Zimbabwe milioni 10.
Nia ya kuingizwa katika noti hiyo katika mzunguko kunatokana na kuzidi kukjosekana kwa fedha kunakotokana na kuzidi kwa mfumuko wa bei.
Pamoja na kuonekana kuwa nyingi, fedha hizo hazitoshi mkate.Kiasi cha mfumuko wa bei kwa sasa ni asilimia 2,200,000.Wataalamu wanasema kiwango cha mfumuko ni zaidi na huo unaoelezwa na Zimbabwe. Asilimia 80 ya wananchi wa Zimbabwe kwa sasa wanaishi katika umaskini mtupu.
Januari mwaka huu Zimbabwe ilitoa noti ya dola milioni 10 na kufuatiwa na dola milioni 50. Hebu soma
cheki BBC



No comments: