Friday, July 18, 2008

BREAKING NEWS - POLISI WAVAMIA MWANAHALISI

Taarifa zilizonifikia hivi punde ni kuwa gazeti la mwanahalisi limevamiwa
muda huu na polisi huku wanaendelea na upekuzi ila hatujui wanataka nini .

Waliwakuta ofisini ndugu Kubenea Said na Ndimara Tegambwagwe pamoja na mlizi
ndugu Mayunga.

Wanaendelea na upekuzi na itakumbuka kuwa hawa hawa ndio ambao walimwagiwa
tindikali na kesi bado inaendelea japo haijulikani nini hatima ya haya mambo
Wamechukua computer ambayo anaitumia pamoja na flash na wameondoka naye
kwenda kumsachi nyumbani kwake na hili lilitokana na kuwa polisi hawa
wanatafuta nyaraka fulani Kuna amri ya mahakama ya kufanya hivyo?

Taarifa tulizo nazo ni kwamba walikuwa wakitafuta nyaraka za benki zilizomuumbua mzee wa vijisenti na kumfanya ajiuzulu hali inayowafanya waingie kiwewe labda na wao siku moja haya mambo yatawakumba.

La maana ni kuwahi mahakamani (kama inawezekana) nadhani ndio sababu wamevamia late today... lakini kama wana search warrant na kama inawapa uwezo wa kwenda kusearch hadi nyumbani.

Upekuzi nyumbani kwake unaendelea na sasa haijulikani nini kinafanyika huko kwani simu yake haipokelewi tena .

Tutawapa yaliyojiri punde.

No comments: