Tuesday, July 29, 2008

Bhoke Munanka

Hayati Isaac Bhoke Munanka enzi za uhai wake
Hihihiiiiii ndivyo wanavyooneana kucheka Rais Mstaafu Mkapa na Aliekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Wake wawili wa marehemu Munanka wakifarijiwa na ndugu na jamaa kabla ya kuuaga mwili wa Munanka unaozikwa jioni hii makaburi ya Kinondoni.


Ndugu na jamaa wa Marehemu Bhoke Munanka wakiomboleza kifo cha ndugu yao huyo kabla ya kuzikwa jioni hii.
Mdogo wa Marehemu Munaka akiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa leo hii nyumbani kwa marehemu Munanka, Kimara Baruti.



Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mohammed Abood akiwa na wambolezaji wengine leo hii nyumbani kwa Munanka, Kimara Baruti. Picha zote za mdau Kassim Mbarouk wa Mwananchi.




Waziri wa Nchi wa zamani katika baraza la kwanza la mawaziri wa Serikali ya awamu ya kwanza Mh. Isaac Bhoke Munanka aliyefariki dunia Jumamosi ilopita akiwa na umri wa miaka 81 anatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Kinondoni, Dar.
Matanga yapo nyumbani kwa marehem huko nyumbani kwake Kimara, Dar.
kwa habari zaidi bofya hapa

No comments: