Friday, October 10, 2014

MAKAMU MWENYEKITI WA NCCR-ZANZIBAR ADONDOKA, AKIMBIZWA AMANA


Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Zanzibar, Haji Ambar Khamis.
MAKAMU Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Zanzibar, Haji Ambar Khamis, leo amedondoka kutokana na matatizo ya moyo na kukimbizwa katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam kwa matibabu.
Baada ya kufikishwa hospitalini hapo, Mhe. Ambar alipimwa na kukutwa presha yake ipo juu ambapo alipelekwa katika chumba namba 7 kwa mapumziko.
Baadaye alipelekwa katika kipimo cha moyo ambapo amekutwa ana tatizo hivyo kushauriwa aanze matibabu mara moja. Mhe. Ambar baadaye aliruhusiwa. SOURCE: GPL

No comments:

WACHIMBAJI WADOGO WAISHUKURU SERIKALI KWA USAMBAZAJI WA UMEME MIGODINI

*Nyang’hwale, Geita* Wachimbaji wadogo wa madini wilayani Nyang'hwale, mkoani Geita, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa...