Friday, October 17, 2014

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI- NISHATI MHE. CHARLES KITWANGA ATEMBELEA MIRADI YA UMEME INAYOFADHILIWA NA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA MKOA WA PWANI

Picha Na 1
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza (aliyesimama mbele) akielezea mchango wa nishati ya umeme katika ukuaji wa uchumi wa mkoa huo, katika kikao chake na Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya  nishati Mhe. Charles Kitwanga. Mhe. Kitwanga  yuko ziarani mkoani humo ambapo anatembelea miradi ya umeme inayofadhiliwa na Wakala wa Nishati  Vijijini (REA) pamoja na kuzungumza na wananchi.
Picha Na 2Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza (kulia) akisisitiza jambo katika kikao hicho. Katikati ni Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga. Kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Tanesco Kanda ya  Dar es  Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mugaya.
Picha Na 3Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga, (aliyesimama) akielezea mikakati ya  Serikali katika kufikisha umeme vijijini katika kikao kilichoshirikisha  Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza  na watendaji wa Tanesco, wataalamu pamoja na waandishi wa habari.
Picha Na 4Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga, akisisitiza jambo katika kikao hicho
Picha Na 5Meneja Mwandamizi wa Tanesco Kanda ya  Dar es  Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mugaya (aliyesimama) akielezea mikakati ya  shirika hilo katika kukabiliana na changamoto ya kukatika kwa umeme kutokana na matengenezo yanayofanyika
Picha Na 6Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika kituo cha umeme cha Chalinze.
Picha Na 8Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga (katikati) akitoa maelekezo kwa wataalamu wa shirika la Tanesco katika kituo cha Chalinze ya jinsi ya kuboresha hali ya umeme katika mji wa Chalinze
Picha Na 11Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga (kushoto) akizungumza na mkazi wa Kiwangwa wilayani Bagamoyo, Said Ramadhani ili kupata maoni yake kuhusiana na utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.
Picha Na 10Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga (katikati) akifurahia jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo,  Ahmed Kipozi (kushoto). Kulia ni Diwani wa Kerege, Tabia Juma.
Picha Na 9Naibu  Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga (katikati) akifurahia jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo,  Ahmed Kipozi (kushoto). Kulia ni Diwani wa Kerege, Tabia Juma.

No comments: