Tuesday, October 28, 2014

KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI YATEMBELEA SUDAN

unnamedWaziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe na Kiongozi wa Kamati ya Bunge ya Kilimo Sudan, Dk. Habib Makhtom wakisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Kurugenzi ya Maandalizi ya Miradi Sudan, Inj. Mohamed Elsheikh.
unnamed2Wajumbe ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, Assa Hamad, Said Nkumba na Abdulsalaam Ameir wakiangalia moja ya mashine zinazotengenezwa katika kiwanda cha GIAD.
unnamed3Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Prof. Peter Msolla, Meneja Mkuu wa kiwanda cha GIAD, Inj. Salah Dafaalla na Mjumbe wa Kamati, Abdallah Ali.
unnamed4Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji wakisikiliza maelezo kutoka kwa moja ya wahandisi katika kituo cha Gridi ya Taifa ya Umeme Sudan.
unnamed5Ujumbe kutoka Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa kituo cha Gridi ya Taifa ya Umeme Sudan.
…………………………………………………………….
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji jana imeanza ziara ya kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa chini ya Ushirikiano wa Nchi za Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiatives) nchini Sudan.
Lengo la ziara hiyo ni kupata uelewa wa pamoja kuhusu ushirikiano uliopo katika kusimamia na kuendeleza rasilimali za Bonde la Mto Nile kati ya Nchi wanachama, huku Tanzania na Sudan zikiwa ni miongoni mwao.
Katika ziara hiyo Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe ambaye ameambatana na kamati hiyo amesema kwamba, dhumuni kuu la ziara hiyo ni kwenda kuona na kujifunza namna Sudan inavyotumia maji ya Mto Nile kwa ajili ya maendeleo yake kiuchumi katika shughuli za kilimo, ufugaji, utalii na biashara.
“Tanzania inachangia asilimia 28 ya maji ya Mto Nile na ina utajiri mkubwa wa rasilimali hii ya maji, hivyo hatuna budi kujifunza kutoka kwa wenzetu ili nasi tupate ufahamu mzuri na tuweze kupata maendeleo makubwa katika nyanja mbalimbali kupitia rasilimali hii. Na hatua ya kwanza ni kuona wenzetu wa Sudan wanafanya nini mpaka kufikia hatua kubwa waliyopiga leo hii”, alisema Prof. Maghembe.
Ziara hiyo ni mwaliko kutoka nchi ya Sudan na itachukua siku nne, itajumuisha kutembelea Bwawa la Merowe linalotumika kwa ajili ya kuzalisha umeme na shughuli za kilimo cha umwagiliaji, inategemewa kuleta tija kwa maendeleo ya Sekta ya Maji nchini na uchumi kwa ujumla.

No comments: