Friday, October 24, 2014

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI AFUNGA MAFUNZO ELEKEZI YA WATUMISHI WAPYA

unnamedMkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Barnabas Ndunguru akimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga (hayupo Pichani) katika ufungaji wa mafunzo elekezi kwa watumishi wapya wa Wizara.Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
unnamed2Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Sihaba Nkinga akiongea na baadhi ya Watumishi wapya wa Wizara katika ufungaji wa mafunzo elekezi yaliyofanyika jijini Dar es Salaam ambapo aliwaasa kuwa na maadili katika utendaji wao wa kazi.
unnamed3Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Sihaba Nkinga katikati akiongea na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Bw. Leonard Thadeo kulia na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Prof. Hermens Mwansoko kushoto mara baada ya kufunga mafunzo elekezi kwa watumishi wapya wa Wizara

No comments: