Monday, March 24, 2008

hongera baba





Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiwa na Spika wa Bunge, Samwel Sitta na mkewe Margareth wakati wa sherehe ya kuadhimisha miaka 40 ya ndoa yao iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mbali na kuhudhuriwa na Rais ambaye alikuwa mgeni rasmi, sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Jaji Mkuu Augustino Ramadhan, Naibu Spika Anna Makinda, Mkuu wa Jeshi la Polisi Said Mwema, Mkuu wa Majeshi Davis Mwamunyange, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Mabalozi pamoja na wabunge. Suala la wanaume kutoa fursa za kujiendeleza kwa wanawake ni mojawapo kati ya masuala makuu ambayo yalijitokeza katika nasaha za wanandoa hao, huku mgeni rasmi akisisitiza juu ya suala la uvumilivu na upendo kuwa ni msingi wa kujenga familia bora. Picha na Jube Tranquilino

No comments:

RAIS SAMIA AZINDUA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA JULIUS NYERERE, AAGIZA UKAMILISHAJI WA MIUNDOMBINU YA KUSAFIRISHA UMEME NCHINI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi, wageni mbalimbali pamoja na wananchi waliohudhur...