




Kikao hicho kimeanza tu muda siyo mrefu baada ya Rais Kikwete kuwa amewasili Butiama tayari kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM .
Kikao cha NEC kinaanza kesho ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika katika kijiji ambako alizaliwa Baba wa Taifa na mwanzalishi wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Rais Kikwete aliwasili Butiama kwa barabara akitokea Mwanza ambako ndege yake ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza mapema asubuhi na akaamua kusafiri kwa gari kwenye Musoma.
Mjini Mwanza, mamia ya wakazi wa mji huo na vitongoji vyake, walijitokeza kwa wingi, katika baadhi ya sehemu za jiji hilo mvua ikiwa inanyesha, kumshangilia Rais wakati msafara wake ukikatisha mitaa ya jiji hilo kuelekea Musoma.
2 comments:
MZEEE MBONA PICHA HAZIONEKANI..NA HUKO DODOMA WANATAMBIKA NINI, TUNATAKA KILA KITU KIENDE KWA UWAAZI NA UKWELII.. MAAANA TUMESHAZIKIA KWAMBA TUMESIMAMISHIWA MISAAADA KUTOKA KWA MATAJIRI...
hivi huk chamwino kuna lipi jipya
Post a Comment