Sunday, March 09, 2008

Mufti Simba mgonjwa

Na Muhibu Said wa Mwananchi

MUFTI wa Tanzania, Sheikh Mkuu, Issa bin Shaaban Simba, amelazwa hospitali mkoani Arusha kwa takriban wiki mbii sasa, akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa kisukari.

Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana, zinaeleza kuwa, Mufti Simba amelazwa katika Hospitali ya Dk Mhando iliyoko mjini Arusha tangu Machi 2, mwaka huu.

Katibu wa Mufti, Sheikh Abdushakur Omar, alilithibitishia gazeti hili juzi na jana kuhusiana na kulazwa kwa Mufti Simba katika hospitali hiyo.Kwa kina zaidi soma Mwananchi la Kesho.

No comments:

SEKTA YA NYUMBA YAPATA MSUKUMO MPYA, NHC YATEKELEZA MIRADI YA MABILIONI NCHINI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo a kiwasilisha  Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ...