Friday, March 14, 2008
Spika aunda upya kamati za bunge
*Muundo wabadilishwa baadhi zaunganishwa
Na Tausi Mbowe wa Mwananchi
SPIKA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta ameteua Kamati Mpya za Bunge na kubadili muundo wa baadhi ya Kamati za awali na kuanzisha kamati mpya.
Katika Muundo huo mpya Spika Sitta ameunganisha baadhi ya Kamati za awali kisha kuanzisha Kamati nyingine mpya nne na kufanya idadi ya Kamati hizo za Bunge sasa kufikia 17 badala ya 13 za awali.
Akizungumza na Mwananchi jana Spika Sitta alisema kuundwa kwa Kamati hizo mpya kunafuatia Kamati za awali kumaliza muda wake. Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Bunge, kamati za Bunge zinatakiwa kufanya kazi kwa miaka miwili na nusu.
Spika Sitta alisema kamati hizo zimegawanyika katika makundi matatu ambayo ni Kamati zisizo za Kisekta, Kamati za Kisekta na Kamati zinazosimamia masuala ya Taarifa za Ukaguzi.
Kanuni za Bunge zinawataka Wabunge kuchagua kwa kuweka alama kulingana na vipaumbele walivyoona inafaa katika Kamati husika. Hata hivyo jukumu la mwisho la kuwachagua Wabunge hao katika Kamati husika ni la Spika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA AFUNGUA SOKO LA KISASA KARIAKOO LILILOGHARIMU BILIONI 28, SASA BIASHARA SAA 24
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Sok...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. . Picha na Jube Tranqu...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
No comments:
Post a Comment