Wednesday, October 17, 2007

'Sekta ya madini haijasaidia Tanzania'

TANZANIA licha ya kuwa na utajiri wa madini bado imeshindwa kunufaika kwa kiwango kikubwa, kutokana na kukosekana mipango iliyowazi katika kudhibiti sekta hiyo.

Akitoa tathimini kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Emanuel Ole Naiko, juu ya Ripoti ya Uwekezaji ya Dunia ya mwaka 2007, Mkurugenzi wa Utafiti na Mawasiliano wa kituo hicho, John Kyaruzi, alisema ipo haja ya kufanyika kazi ya ziada kuona madini yanatumika kupunguza umasikini kwa Watanzania.

Kyaruzi alifafanua kwamba baadhi ya makampuni yanayochimba madini yamekuwa na ajenda zao za kibiashara na kwamba kazi kubwa kwa serikali ni kutokubaliana na mambo yasiyo na manufaa kwa nchi.

Alifafanua kwamba, sekta ya madini imekuwa ikitarajiwa kufungua milango zaidi ya uwekezaji wa moja kwa moja (FDI) na kusaidia nchi zenye utajiri huo kuendelea, lakini kwa Tanzania bado haijafanya vizuri hasa katika mipango.
Bonyeza GAZETI LA MWANANCHI upate taarifa zaidi.

No comments: