Monday, October 22, 2007

Chissano anyakua tuzo ya Mo Ibrahim


RAIS mstaafu wa Msumbiji Joaqium Chissano, amewabwaga Marais wengine 12 akiwemo Benjamin Mkapa wa Tanzania, katika kinyang'anyiro cha Tuzo ya Rais bora wa Afrika.

Ushindi wa Chissano umetangazwa mjini London jana na Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa (UN), Kofi Annan.

Tuzo hiyo ambayo imetolewa na Taasisi ya Mohamed Ibrahim, bilionea mzaliwa wa Sudan, msingi wake ni mambo matatu, Kukuza Demokrasi, Utawala Bora na Maendeleo katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.

No comments:

Rais Dkt. Samia Awasili Addis Ababa Kushiriki Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi wa AU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bole, Jij...