Rais Jakaya Kikwete ameonya tabia inayotaka kujengeka miongoni mwa wananchi na hususani wanasiasa ya kugeuka kuwa wapelelezi, wakamataji, waendesha mashtaka na watoa hukumu, na tena wakizitoa huku hizo bila ya watuhumiwa kuwapo.
Amesema tabia hiyo ikiachwa kuendelea siyo tu itaipeleka nchi pabaya, lakini itawatisha wananchi, itawatia hofu na kujenga chuki kati ya mtu na mtu hali ambayo amesema haiendani na taratibu za kuendesha nchi kwa misingi ya kufuata kanuni, taratibu, na sheria za nchi.
Amebainisha kwamba tabia hiyo ya wanasiasa kujigeuza kuwa wao ndio wapelelezi, wakamataji, waendesha mashtaka na watoa hukumu kuwa haimtendei haki mtuhumiwa ambaye naye ana haki yake ya msingi ya kulindwa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Rais Kikwete ameeleza kuwa kila taarifa inayohusu rushwa au tuhumu za mtu kutuhumiwa kuhusika na vitendo vya rushwa, zitachunguzwa kwa kuzingatia misingi ya sheria za nchi na vyombo vinavyohusika na si vinginevyo na kuongeza kwamba yeyote atakayethibitishwa na mamlaka halali kwamba ama ametoa rushwa au kupokea rushwa atachukuliwa hatua za kisheria bila ya kujali nafasi na madaraka aliyonayo. ukitaka kusoma zaidi cheki TAARIFA YA IKULU HAPA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Afisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu we...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment