MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kagera imemwachia huru Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatale, katika shtaka lililokuwa likimkabili la kumshambulia na kumjeruhi Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Renatus Mutabuzi, kwa sharti la kutotenda kosa lolote la jinai ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu wa Mkazi wa mahakama hiyo, Cleophace Waane, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashtaka na kwa kuzingatia maombi ya wakili wa mshtakiwa huyo, Twaha Tasilima, yaliyotolewa kabla ya hukumu hiyo kutolewa.
Akisoma hukumu hiyo, hakimu Waane alisema kuwa mahakama imeona baadhi ya maombi yaliyoombwa na wakili wa mshtakiwa ambayo aliomba yazingatiwe na mahakama wakati wa kutoa hukumu ni ya muhimu, hivyo kuamua kutoa adhabu ndogo kwa mshtakiwa huyo. Bonyeza GAZETI LA MWANANCHI upate taarifa zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Prof. Mfaransa Aja na Kitabu: Aiambia Dunia Kutalii Tanzania ni Tiba
Na Mwandishi Wetu Paris, Ufaransa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana, akiwa nchini Ufaransa jana Julai 8, 2025 amek...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
No comments:
Post a Comment