Thursday, December 18, 2014

BALOZI MARMO AKABIDHI HATI ZA UTAMBULISHO KWA RAISI WA AUSTRIA

Botschafter von Tansania Philip Sang'ka Marmo
Balozi wa Tanzania nchini Austria ambaye ana makazi mjini Berlin, Ujerumani Mhe. Philip S. Marmo; mapema mwezi huu alikabidhi Hati za Utambulisho (Letter of Credence) kwa Mhe. Dkt. Heinz Fischer, Rais wa Austria. Shughuli hizi zilifanyika katika ukumbi maarufu wa Maria Teresa uliopo katika kasri ya wafalme wa zamani wa “Austro-Hungarian Empire” mjini Vienna. Gwaride rasmi kwa ajili ya Balozi mpya iliendeshwa katika viwanja vya Hofburg.
Botschafter von Tansania Philip Sang'ka Marmo
Balozi wa Tanzania nchini Austria ambaye ana makazi mjini Berlin, Ujerumani Mhe. Philip S. Marmo akipokea heshima kutoka Gwaride rasmi kwa ajili ya Balozi huyo ambalo katika hafla ambayo  iliendeshwa katika viwanja vya Hofburg.
balozi_wa_tanzania_philip_marmo_na_raisi_wa_uswissi_didier_burkhalter_2014aMhe. Balozi Philips S. Marmo, Balozi  wa Tanzania nchini Uswissi mwenye makazi mjini Berlin, Ujerumani hivi karibuni alikabidhi Hati za Utambulisho (Letters of Credence)kwa Mhe. Didier Burkhalter, Rais wa Shirikisho wa Serikali ya Uswissi na kufanya maongezi na Mhe. Rais akiwa ameandamana na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Uswissi.
balozi_wa_tanzania_philip_marmo_na_raisi_wa_uswissi_didier_burkhalter_2014bMhe. Balozi Philips S. Marmo, Balozi  wa Tanzania nchini Uswissi mwenye makazi mjini Berlin, Ujerumani akiwa katika mazungumzo na Mhe. Didier Burkhalter, Rais wa Shirikisho wa Serikali ya Uswissi.

No comments: