Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika, Oktoba 7, 2014, katika Kijiji cha Magozi, Kata ya Ilolo Mpya, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM katika jimbo la Isimani la Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge, William Lukuvi katika wilaya ya Iringa Vijijini, mkoani Iringa. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-ISIMANI-IRINGA)
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Lukuvi wakishiriki kufyatua matofali ujenzi wa Zahanati Kijiji cha Magozi Ilolo Mpya
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Magozi, Kata ya Ilolo Mpya akiwa katika ziara ya kikagua utekelezaji wa ilani ya CCM katika jimbo la Isimani, wilaya ya Iringa Vijijini. Kushoto ni Mbunge wa jimbo hilo, William Lukuvi
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsisitizia jambo Lukuvi baada ya kukagua ujenzi wa zahanati hiyo kutoka kshoto ni Hassan Mtenga Katibu wa CCM mkoa wa Iringa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya sekondari William Lukuvi Ilolo Mpya.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano huo
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akieleza sera za Chama wakati akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuzungumza na wananchi kwenye mkutano huo
Mjumbe wa shina namba sita, Changula Mlula akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwenye kikao cha shina hilo, Kijiji cha Magozi, Ilolo Mpya jimbo la Isimani. Kulia ni Mbunge wa Isimani William Lukuvi
Wananchi wa Jamii ya Kimasai wakicheza ngoma kumpokea Kinana wakati wa mkutano huo
Mbunge wa Isimani, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge, William Lukuvi akieleza alivyotekeleza ilani ya CCM wakati wa mkutano huo
Mbunge wa Isimani William Lukuvi akiwa amemkabidhi kompyuta Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya Pawaga Bw. Yusuph Luvanga
Wananchi wa Jamii ya Wasukuma wakicheza ngoma kumlaki Kinana kwenye mkutano huo
Lukuvi akiselebuka na wananchi katika kucheza ngoma wakati wa mapokezi ya Kinana kwenye mkutano huo
Msanii Nyamidela akitumbuiza na wimbo wake maalum unaomzungumzia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpongeza msanii Nyamidela mara baada ya kutumbuiza
Mbunge wa Isimani William Lukuvi akiwa amemkabidhi kompyuta Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya William Lukuvi, iliyopo Kata ya Ilolo Mpya, Charles Mgimwa (kulia ) wakati wa mkutano huo. Mbali na kuwakabidhi kompyuta walimu wa shule mbili za sekondari aliwataka wananchi kuwa tayari kuunganishiwa umeme wa bei nafuu ambao alisema utaaingia kwenye kata hiyo hivi karibuni.
Mmoja wa wananchi akiuliza swali
No comments:
Post a Comment