Thursday, August 01, 2013

UNIC YAHAMASISHA VILABU VYA KUJISOMEA KWA SHULE ZA MSINGI

.IMG_1445

Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini

 (UNIC) Stella Vuzo akielezea jukumu lao kubwa wao kama Unic ni
 kuelimisha jamii ambapo kwa kufanya hivyo wamehamasika kuanzisha 
vilabu vya kujisomea kwa shule za msingi vitakavyowajengea watoto
 msingi mzuri wa kupenda kujisomea ili kufahamu mambo mengi zaidi 
yanayoendelea duniani katika nyanja ya Sayansi, Teknolojia na habari.
IMG_1488

















Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha ( wa tatu kushoto)

na Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki katika 
kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni 
Mama Demere Kitunga ( wa nne kushoto) wakikabidhi vitabu vya 
kujisomea kwa  walimu na baadhi ya wanafunzi wa shule ya 
msingi Oysterbay jijini Dar es Salaam.


IMG_1498

















Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) 
Stella Vuzo akishiriki zoezi hilo la kukabidhi vitabu kwa baadhi ya wanafunzi 
wa shule ya Msingi Oysterbay wakihamasisha wanafunzi kujenga tabia ya
 kujisomea tangu wakiwa wadogo.
IMG_1494

















Afisa Habari wa UNIC Usia Nkhoma Ledama naye alishiriki zoezi hilo.
IMG_1508

















Mwalimu Salome Makanza (kushoto) akitoa shukrani kwa kituo cha
 habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) kwa msaada huo ambapo
 waliahidi kuleta mabadiliko ya maendeleo kwa wanafunzi wao kujijengea
 tabia ya kujisomea na hata kuongeza ufaulu kwa matokeo ya darasa la 
saba shuleni hapo. Katikati ni Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet 
Macha na kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki 
katika kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni 
Mama Demere Kitunga.
IMG_1398

















Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha akitoa ushauri wa 
namna ya upangaji vitabu kwa Msimamizi wa Maktaba ya shule 
hiyo Mwl. Veronica Kassidy.
IMG_1401

















Unic team wakijikumbushia baadhi ya vitabu walivyowahi kuvisoma 
walipokuwa shule za msingi.
IMG_1415

















Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Oysterbay wakichagulia 
vitabu vya kujisomea katika maktaba ya shule yao.
IMG_1513 
















Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki katika 
kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni 
Mama Demere Kitunga na Afisa Habari wa UNIC Stella Vuzo 
wakiteta jambo na baadhi ya wanafunzi wa shule mara baada 
ya kumaliza zoezi la kukabidhi vitabu wanafunzi hao.

No comments: