Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando akizungumza wakati wa kuchezesha droo ya kusaka mshindi wa nyumba wa kwanza kupitia Promosheni ya Airtel Yatosha. Kushoto ni Msimamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bw. Mrisho Milao, kulia ni Meneja Masoko wa Airtel, Aneth Muga wa kwanza kulia. Droo ya Airtel Yatosha ilimpata mshindi wa Nyumba Bw Silvanus Juma kutoka mkoa wa Iringa.
Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando, Msimamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bw. Mrisho Milao (kushoto) na Meneja Masoko wa Airtel, Aneth Muga wa kwanza kulia wakisubiri draw ya kutafuta mshindi itafute namba ya mshindi wakati wa kutafuta mshindi wakati wa kuchezesha droo ya kusaka mshindi wa nyumba wa kwanza kupitia Promosheni ya Airtel Yatosha. Droo ya Airtel Yatosha ilimpata mshindi wa Nyumba Bw Silvanus Juma kutoka mkoa wa Iringa.
Meneja Masoko wa Airtel, Aneth Muga wa kwanza kulia akizungumza na simu ya mshindi wa nyumba ya kwanza ya Airtel wakati wa kutafuta mshindi wakati wa kuchezesha droo ya kusaka mshindi wa nyumba wa kwanza kupitia Promosheni ya Airtel Yatosha katikati ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando na  Msimamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bw. Mrisho Milao (kushoto) . Droo ya Airtel Yatosha ilimpata mshindi wa Nyumba Bw Silvanus Juma kutoka mkoa wa Iringa.
                          **************************************88 
Airtel
 Tanzania imetangaza mshindi wa kwanza wa nyumba  kupitia promosheni ya 
Airtel Yatosha Shinda nyumba inayoendelea  na kuwazawadia wateja wake 
kila siku Bwana Silvanus Juma mkazi wa Iringa mwenye umri wa miaka 33 
ambaye ni mhasibu katika shirila la Tanzania Rural women and children 
development foundation - TARWOC ameibuka mshindi na kuzawadiwa  nyumba 
kisasa iliyojengwa na shirika na nyumba la taifa NHC iliyopo kigamboni
jijini Dar es Saalam.
Akiongea wakati wa kuchezesha droo hiyo Meneja Uhusiano wa Airtel 
bwana Jackson Mmbando alisema" kama tulivyowangazia awali leo ndio ile 
siku muhimu na maalumu ya kumpata mshindi wetu wa kwanza wa nyumba  na 
tumeshuhudia bwana Silvanus Juma  akiibuka mshindi kupitia droo ya 
kwanza tuliyoichezesha hapa.
Sambaba na hilo leo tunao washindi 7 wa wiki  kutoka katika mikoa 
mbalimbali ambao hawa wataondoka na pesa taslimu shilingi  milioni moja 
kila moja, washindi hawa ni pamoja na  Peter Ignasho kutoka Muheza 
Tanga, Edita Rweyabura  kutoka Bukoba, Steven Maguro , Rakesh Ali Mauji,
 Mwajuma Hassani kutoka Dar es Saalam, Siasa Yahaya Songo kutoka Manyoni
 Singida and Vero Mispela Kiwango kutoka Bihalamulo.
Natoa wito kwa watanzania na wateja wetu kuendelea kutumia huduma ya 
Airtel yatosha na kujiunga na vifurushi mbalimbali na kupata nafasi ya 
kujishindia zawadi mbalimbali , kujiunga nirahisi piga  *149*99# kisha 
nunua kifurushi chacko cha  siku, wiki au mwezi  na kisha kuingizwa moja
 kwamoja kweny droo ya kuweza kushinda milioni moja kila siku au zawadi 
kubwa ya Nyumba.
Akiongea mara baada ya kutangazwa mshindi Bwan Silvanus Juma 
alisema"Ninayofuraha sana kupata zawadi hii kubwa kutoka Airtel napenda 
kutoa wito kwa watanzania na wateja wa Airtel waendelee kutumia huduma 
ya Airtel yatosha na waamini kuwa hakuna upendeleo.
Binafsi sijawahi kushinda Bahati nasibu yoyote na nilikuwa siamini 
kama hakuna ubaguzi kwenye kushinda, lakini leo nashuhudia kwamba 
ushindi ni wa uhakika usio na upendeleo wala ubaguzi hivyo wajaribu nao 
wanaweza kuwa washindi.
Kwa upande wake moja ya wafanyakazi wenzake Bwana Beatus Magoti 
ambaye ni Mshauri wa fedha na utawala TARWOC alisema"  tumefurahi sana 
kuona kijana mgodo mwenzetu ambaye ni mchapa kazi ameweza kushinda 
nyumba kupitia promosheni ya Airtel yatosha.  Hii imetupa hamasa na sisi
 kushiriki na kueneza habari kwa wengine kushiriki na kushinda kama
laivyoshinda Silvano.
Airtel inaendelea na promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba tatu 
ikiwa na lengo la kuwazawadia wateja wake na kutoa huduma bora zenye 
gharama nafuu kupitia huduma ya Airtel yatosha.  Sambamba na hilo Airtel
 pia imewawezesha wateja wake nchi nzima  kutuma na kutoa pesa bure bila
 makato yoyote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...
- 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
 - 
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
 - 
(Picha na Yahya Charahani) Katika kijiji cha Mwanjoro, wilayani Meatu – Shinyanga, maisha bado yanapumulia kwenye nyumba za udongo na mapaa...
 
No comments:
Post a Comment