Friday, August 16, 2013

MWINGINE ANASWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE DAR‏

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akionesha picha ya

 kijana Leonard Jeremiah Monyo (Edwin Jeremiah Monyo) ambaye 
amekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya kwa wanahabari.…
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akionesha picha ya kijana
 Leonard Jeremiah Monyo (Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa
 na kete 86 za madawa ya kulevya kwa wanahabari.

Wanahabari wakimsikiliza Dk. Mwakyembe.

JUHUDI za Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe za 
kupambana na dawa za kulevya nchini Tanzana zimeanza kuzaa 
matunda baada ya jana akiwa katika ukaguzi wa Kiwanja cha Ndege 
cha Kimataifa Julius Nyerere kunaswa kijana akijaribu kupita na 
dawa za kulevya katika uwanja huo.

Kwa kile kuoneshwa kukerwa na tabia hizo, Dk. Mwakyembe 
amempiga picha kijana huyo ambaye ni rasta na pita yake itasambazwa
 maeneo tofauti, huku kesi yake ikiendelea ya kupatikana na madawa 
hayo ya kulevya.

Akizungumza na vyombo vya habari leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam
, Dk. Mwakyembe alimtaja kijana aliyekamatwa jana kuwa ni Leonard 
Jeremiah Monyo (Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa na kete 
86 za madawa ya kulevya aina ya heroin akitaka kusafiri nazo kuelekea 
misokoto ya bangi 34 akiwa ameficha kwenye begi lake.

Alisema kijana huyo rasta alinaswa na mtambo wa kukagua mzigo baada 
ya wakaguzi kuushuku mzigo wake hivyo kuamuru ukaguliwe ndipo 
alipokutwa na madawa hayo haramu akijaribu kusafiri nayo kwa ndege.
Alisema kijana huyo kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa uchunguzi
 zaidi kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kukutwa na dawa
 hizo haramu. Alisema kwa kile kuoneshwa kukerwa na vitendo hivyo na 
kuamua kwa dhati kupambana navyo wamempiga picha kijana huyo na picha
 zake zitasambazwa maeneo mbalimbali ili aonekane na umma kujua watua 
ambao wamekuwa wakilichafua taifa nje na ndani kutokana na biashara hizo 
haramu.

Dk. Mwakyembe amesema atahakikisha anafuatilia kesi ya kijana huyo 
hadi itakapoishia ili uona hatua za kisheria zinachukuliwa kwa wahusika
 na vitendo hivyo kukomeshwa. Alisema maofisa wakaguzi wa mizigo 
wawili (wote wasichana) ambao walimnasa kijana huyo watazawadiwa
 na kupandishwa daraja kutokana na kazi nzuri waliyoifanya.

"Jana tu baada ya ukaguzi wenzetu ambao wanaona kama tunafanya mzaha
 jana tena wakapitisha mzigo wa madawa ya kulevya kiwanja cha ndege cha
 Dar es Salaam, kwa sababu vijana wetu sasa wameamka na hawataki mchezo 
wakamkamata kijana huyo...," alisema.

"Picha yake itasambazwa kila sehemu...sidhani kama tunahitaji upelelezi kwa
 sababu tumekukamata na dawa za kulevya. Mimi na viongozi wangu kupitisha
 dawa za kulevya akikisha kuuhakikisha.

Alisema kijana huyo alikamatwa majira ya saa mbili na nusu usiku akiwa anasafiri 
kwenda nchini Italia kwa kutumia ndege ya kampuni ya Swissair. Alisema kwa sasa kila atakayekamatwa na dawa za kulevya picha yake itasambazwa maeneo mbalimbali ya
 nchi ili watu hao wajulikane.

Alisema kwa sasa taratibu zinafanywa ili kuhakikisha mizigo ya abiria wanaowasili 
kutoka nje ya nchi kuingia Tanzania nao mizigo ikaguliwe ili kuwabaini wanaoingiza
 bidhaa hiyo haramu ichini pia. Aliongeza zoezi hilo litafanyika katika viwanja vya 
ndege na bandarini kwa kila mizigo inapowasili.

Alisema lengo ni kuhakikisha viwanja vya ndege vinakuwa salama na kuacha 
kutumika vibaya na baadhi ya watu, jambo ambalo limeendelea kulichafua taifa.
 Alisem kiwanja cha Dar es Salaam ni kizuri na kina vifaa vya usalama vya kutosha
 ila mapungufu yaliyopo ni kwa baadhi ya wafanyakazi ambao wanatumia vibaya 
madaraka yao.

Dk. Mwakyembe ameahidi kuwataja na kuweka picha zao hadharani watu ambao
 wanajihusisha na madawa hayo ya kulevya. Amesema wanatarajia kutaja majina 
ya Watanzania ambao hivi karibuni walinaswa na dawa za kulevya nchini Afrika 
Kusini katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo. Alisema Watanzania wengine 
wamekamatwa Hong Kong wakihusishwa na dawa hizo na wanafuatilia pia picha 
na majina yao yatawekwa hadharani muda wowote. 

No comments: