Monday, August 05, 2013

JAJI FRANCIS MUTUNGI ATEULIWA KUWA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI

Msajili wa Vyama vya Siasa mpya, Jaji Francis S.K.Mutungi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho 
Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili 
wa Vyama vya Siasa.
Taarifa iliyotolewa Dar Es Salaam leo, Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa 
saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi 
huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.
Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa 
Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma
 kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
 Kanda ya Dodoma.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

No comments: