Friday, August 30, 2013

MWANAMUZIKI DIAMOND AMKABIDHI GARI MWANAMUZIKI MKONGWE(MSTAAFU)MZEE MUHIDIN GURUMO,KATIKA HAFLA YA UZINDUZI WA VIDEO YAKE


 Mwanamuziki Diamond Platnum akimkabidhi funguo ya gari aina ya 
Toyota Funcargo mwanamuziki mkongwe nchini mzee Muhidin Gurumo 
kama zawadi yake kwa mkongwe huyo wa muziki baada ya kustaafu rasmi 
kuimba muziki, Diamond alitoa zawadi hiyo kwa Gurumo katika hafla 
yake ya uzinduzi wa video yake mpya ya wimbo Nomber One aliyoirekodi
 huko Afrika Kusini ikigharimu kiasi cha dola elfu 30.000 zaidi ya milioni 
arobaini za Tanzania, Video hiyo imetengenezwa kwa viwango vya kimataifa 
na itaweza kumtangaza vyema kijana huyo wa kitanzania katika ulimwengu 
wa muziki hasa kimataifa, Hafla hiyo imefanyika kwenye hoteli ya Serena 
Dar es salaam na imehudhuriwa na wasanii pamoja na waigizaji wa filamu
 na watu maarufu mbalimbali
 Mzee  Muhidin Gurumo akimshukuru Diamond kwa kumzawadia gari jambo ambalo kwake ni kama ndoto kwakuwa amestaafu akiwa hana usafiri “Yaani sijui hata mke wangu nikimwambia atanielewaje manake ni jambo la kushangaza kwangu” Alisema mzee Gurumo
 Diamond akimuongoza mzee Gurumo kwenda kumuonyesha gari
 Diamond akimuonyesha Mzee Gurumo gari
Akimuelekeza jambo baada ya mzee Gurumo kuingia kwenye gari
 Mzee Gurumo akihojiwa na waandishi wa habari
 Kulia ni Irene Uwoya kushoto Salma Msangi
 Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiwa na mama yake Diamond
 Kutoka kulia ni Raymond Kigosi, Irene Uwoya na JB wakiwa katika hafla hiyo.
 Wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo. Picha zote na John Bukuku

No comments: