Thursday, July 04, 2013

KAMPUNI YA EAG GROUP WATENGENEZAJI WA SIMU ZA SMARTPHONE AINA YA MOTEK WANAWAKARIBISHA KUTEMBELEA BANDA LAO LILILOPO KATIKA VIWANJA VYA SABASABA JIJINI DAR ES SALAAM


Banda la EAG Group ndani ya Viwanja vya maonyesho ya Sabasaba linavyoonekana
 Mfanyakazi wa Kampuni ya EAG Group Annie Moses, Ambao ni watengenezaji na wauzaji wa Simu aina Ya Motek na Milango Kutoka Nchini Tanzania akitoa maelezo kwa Mteja aliyefika Kwaajili ya Kutaka Kununua Simu aina ya Motek katika Banda la EAG Group lililopo ndani ya Viwanja vya Sabasaba
 Moja ya Mlango unaotengenezwa Na Kampuni ya EAG Group ukiwa ndani ya banda lao lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba kwaajili ya Maonyesho.Kampuni ya EAG Group ni moja ya Kampuni za Kitanzania ambayo inahusika na Utengenezaji wa Simu aina Za Smartphone aina ya  Motek na milango inayotumika kwaajili ya usalama kama inayoonekana katika Picha
 Mfanyakazi wa Kampuni ya EAG Group Saima Seif akitoa maelezo kwa mteja aliyefika katika banda la EAG Group lililopo ndani ya Viwanja vya Sabasaba kwaajili ya kununua Simu aina ya Motek inayotengenezwa na Kuuzwa na Kampuni hiyo
 Mfanyakazi wa Kampuni ya EAG Group Bw Ramadhan Athuman akitoa maelezo kwa mmoja wa wateja waliofika katika Banda lao lililopo ndani ya Viwanja vya Sabasaba kwaajili ya kupata maelezo juu ya aina ya Milango inayotengenezwa na Kampuni hiyo ya EAG Group
 Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya EAG Group wakiwahudumia wateja waliofika katika banda lao lililopo kwenye viwanja vya Sabasaba kwaajili ya kununua simu aina ya Motek
 Mfanyakazi wa Kampuni ya EAG Group Upendo Shirima akimuuzia mteja Simu aina ya Motek wakati mteja huyo alipifika katika banda la kampuni ya EAG Group lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba jijini Dar Es Salaam.Picha Na Josephat Lukaza

No comments: