Monday, July 22, 2013

WAANDISHI WATEMBELEA NYUMBA 3 ZA AIRTEL YATOSHA - KIGAMBONI

Baadhi ya waandishi wa vyombo vya habari nchini walipotembelea moja kati ya Nyumba 3 zinazotarajiwa kutolewa katika promosheni ya AIRTEL YATOSHA  mwishoni mwa mwezi huu. Nyumba hizi ziko wilaya ya Temeke eneo la Kibada ambapo zimenunuliwa na Airtel toka shirika la nyumba la taifa kwa ajili ya promosheni ya AIRTEL Shinda Nyumba 3.
Meneja Mawasiliano wa shirika la nyumba la  Taifa, Bw. Yahya Charahani  akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati ambapo waandishi hao walitembelea eneo la Kibada wilaya ya Temeke kujionea Nyumba 3 zinazoshindaniwa katika promosheni ya Airtel Yatosha. Nyumba hizi zimenunuliwa na Airtel toka shirika la nyumba la taifa kwa ajili ya promosheni ya AIRTEL Shinda Nyumba. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando.
Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati ambapo waandishi hao walitembelea eneo la Kibada wilaya ya Temeke kujionea Nyumba 3 zinazoshindaniwa katika promosheni ya Airtel Yatosha.

Mmoja wa waandishi wa Habari wa ITV/Radio One, Bw Juma Kapalatu akiwapongeza Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando (kulia) na Meneja Mawasiliano wa NHC, Bw.Yahya Charahani (katikati) mara baada ya kujionea baadhi ya nyumba zinazoshindaniwa na wateja wa Airtel. 
WAANDISHI WATEMBELEA NYUMBA 3 ZA AIRTEL YATOSHA - KIGAMBONI
•  Wathibitishiwa na NHC Nyumba 3 za Airtel Yatosha zitakuwa tayari mshindi akipatika
•   Mshindi wa kwanza wa Nyumba ya YATOSHA kupatikana mwishini mwa mwezi huu
Mwishoni mwa wiki Shirika la nyumba la taifa limewathibitishia Watanzania kwamba tayari nyumba tatu zinazoshindaniwa katika promosheni ya Airtel Yatosha zimekamilika na tayari mafundi wanafanya matengenezo ya mwisho tayari kwa kukabidhiwa kwa washindi hao.
Meneja Mawasiliano wa NHC YAHYA CHARAHANI amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati ambapo wanahabari toka vyombo mbalimbali walitembelea nyumba hizo kujionea jinsi mradi unavyokwenda “nyumba hizi tatu zenye thamani ya shilingi milioni 194 zimekamilika na pindi washindi watakapotangazwa wataweza kuhamia katika nyumba hizi mara moja tu.
Amesema nyumba hizo ambazo ni za kisasa zitakidhi mahitaji ya wengi kwani ujenzi wake umezingatia mahitaji ya familia kubwa.
Nyumba hizi zina vyumba vitatu vya kulala, jiko, sebule nzuri pamoja na sehemu ya nje iliyonakishiwa kwa umakini ili kuipa nyumba mvuto wa hali ya juu. Aliongeza Bw, CHARAHANI Pia alibainisha kuwa wateja wa kampuni ya Airtel wanaweza kuzitembelea
nyumba hizo na kujionea wenyewe kiwango cha ubora wa nyumba hizo.
“Hizi nyumba ziko wilaya ya Temeke eneo la kibada karibu kabisa na Tuangoma ambapo hadi kufika katika nyumba hizi ni umbali wa kilomita 2 tu kutoka kituo cha basi kilipo, eneo ambalo linafikika na lina makazi mzuri sana,” alimalizia kwa kusema Bw, CHARAHANI.
Naye Meneja Uhusiano wa Airtel JACKSON MMBANDO amewataka watanzania kuendelea kutumia mtandao wa Airtel hususani huduma ya yatosha kwa kupiga *149*99# na kuchagua vifurushi vinavyowatosha  ili kujihakikishia nafasi ya kushinda nyumba hizo.

Amesema Airtel imedhamilia kutatua matatizo ya wateja wake kwa kutoa huduma nafuu na bora kuliko mtandao wowote lakini pia  promosheni hiyo ya YATOSHA  inalenga kubadilisha maisha ya watanzania hasa wale wanaotumia mtandao wa airtel
Amesema katika promosheni hiyo jumla ya shilling million 284 zitatumika kuwazadia wateja wa kampuni hiyo ambapo milioni 194
zitanunua nyumba hizo 3 toka shirika la nyumba na kiasi kinachobaki kwa siku 90 Airtel itatoa milioni moja kwa mshindi mmoja kila siku.

No comments: