Wednesday, July 24, 2013

Mwonekano wa leo wa nyumba za gharama nafuu NHC Mkinga


 Vijana wakiwa kazini kuendelea na ufyatuaji wa matofali , kwa mbali (mwenye shati ya njano na nyeusi) anaonekana Muungano Kasibi Saguya, Meneja Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa.
 Matofali yaliyofyatuliwa na Brigade ya vijana wa Veta waliopata mafunzo kutoka Mkufunzi wa Hydraform Afrika Kusini, matofali haya yanafyatuliwa mfululizo yote hadi yanapokamilika, idadi ikitimia vijana wanaondoka wanahama na mashine yao kwenda kwenye mradi mwingine.
Mwonekano wa sasa wa nyumba za gharama nafuu zinzzojengwa eneo la Kasera-Mkinga wilayani Mkinga mkoani Tanga nyumba hizi ziko takribani 50

Sehemu ya nyuma ya nyumba za gharama nafuu ya nyumba hizo inavyoonekana wakati ujenzi ukiwa unaendelea.

No comments:

WIZARA YA AFYA YAOMBA SH. TRILIONI 1.8 BAJETI YA 2026/2027

  Wizara ya Afya imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma z...